Hes. 3:48-51 Swahili Union Version (SUV)

48. na hizo fedha ambazo waliosalia wamekombolewa kwazo utampa Haruni na wanawe.

49. Basi Musa akawatoza fedha za ukombozi, hao waliozidi hesabu ya wale waliokombolewa na Walawi;

50. akatwaa hizo fedha kwa wazaliwa wa kwanza wa wana wa Israeli; shekeli elfu moja na mia tatu na sitini na tano kwa shekeli ya mahali patakatifu;

51. kisha hizo fedha za ukombozi Musa akampa Haruni na wanawe, kama neno la BWANA, kama BWANA alivyomwagiza Musa.

Hes. 3