Hes. 27:9-12 Swahili Union Version (SUV)

9. Tena ikiwa hana binti, mtawapa nduguze urithi wake.

10. Na ikiwa hana ndugu, mtawapa ndugu za babaye huo urithi wake.

11. Tena ikiwa babaye hana ndugu, utampa huyo aliye karibu naye katika jamaa zake huo urithi wake, naye atakuwa nao; na neno hili litakuwa ni amri ya hukumu kwa wana wa Israeli, kama BWANA alivyomwagiza Musa.

12. BWANA akamwambia Musa, Panda wewe juu ya mlima huu wa Abarimu, uitazame nchi niliyowapa wana wa Israeli.

Hes. 27