Hes. 26:9-16 Swahili Union Version (SUV)

9. Na wana wa Eliabu; Nemueli, na Dathani, na Abiramu. Hawa ndio Dathani na Abiramu waliochaguliwa na mkutano, ambao walishindana na Musa na Haruni katika mkutano wa Kora, hapo waliposhindana na BWANA;

10. nchi ikafunua kinywa chake, na kuwameza pamoja na Kora, mkutano huo ulipokufa; wakati moto ulipowateketeza watu mia mbili na hamsini, nao wakawa ishara.

11. Pamoja na hayo, hao wana wa Kora hawakufa.

12. Na wana wa Simeoni kwa jamaa zao; wa Yemueli, jamaa ya Wayemueli; wa Yamini, jamaa ya Wayamini; na Yakini, jamaa ya Wayakini;

13. wa Sohari, jamaa ya Wasohari; wa Shauli, jamaa ya Washauli.

14. Hizi ndizo jamaa za Wasimeoni, watu ishirini na mbili elfu na mia mbili.

15. Na wana wa Gadi kwa jamaa zao; wa Sifoni, jamaa ya Wasifoni; wa Hagi, jamaa ya Wahagi; wa Shuni, jamaa ya Washuni;

16. wa Ezboni, jamaa ya Waezboni; wa Eri, jamaa ya Waeri;

Hes. 26