Hes. 26:6-20 Swahili Union Version (SUV)

6. na wa Hesroni, jamaa ya Wahesroni; na wa Karmi, jamaa ya Wakarmi.

7. Hizi ndizo jamaa za Wareubeni; na hao waliohesabiwa kwao walikuwa arobaini na tatu elfu na mia saba na thelathini.

8. Na wana wa Palu; Eliabu.

9. Na wana wa Eliabu; Nemueli, na Dathani, na Abiramu. Hawa ndio Dathani na Abiramu waliochaguliwa na mkutano, ambao walishindana na Musa na Haruni katika mkutano wa Kora, hapo waliposhindana na BWANA;

10. nchi ikafunua kinywa chake, na kuwameza pamoja na Kora, mkutano huo ulipokufa; wakati moto ulipowateketeza watu mia mbili na hamsini, nao wakawa ishara.

11. Pamoja na hayo, hao wana wa Kora hawakufa.

12. Na wana wa Simeoni kwa jamaa zao; wa Yemueli, jamaa ya Wayemueli; wa Yamini, jamaa ya Wayamini; na Yakini, jamaa ya Wayakini;

13. wa Sohari, jamaa ya Wasohari; wa Shauli, jamaa ya Washauli.

14. Hizi ndizo jamaa za Wasimeoni, watu ishirini na mbili elfu na mia mbili.

15. Na wana wa Gadi kwa jamaa zao; wa Sifoni, jamaa ya Wasifoni; wa Hagi, jamaa ya Wahagi; wa Shuni, jamaa ya Washuni;

16. wa Ezboni, jamaa ya Waezboni; wa Eri, jamaa ya Waeri;

17. wa Arodi, jamaa ya Waarodi; wa Areli, jamaa ya Waareli.

18. Hizi ndizo jamaa za wana wa Gadi kama waliohesabiwa kwao, arobaini elfu na mia tano.

19. Na wana wa Yuda, Eri na Onani; na hao Eri na Onani wakafa katika nchi ya Kanaani.

20. Na wana wa Yuda kwa jamaa zao; wa Shela, jamaa ya Washela; wa Peresi, jamaa ya Waperesi; wa Zera, jamaa ya Wazera.

Hes. 26