Hes. 25:9-12 Swahili Union Version (SUV)

9. Nao waliokufa kwa hilo pigo walikuwa watu elfu ishirini na nne hesabu yao.

10. Kisha BWANA akanena na Musa, akamwambia,

11. Finehasi, mwana wa Eleazari, mwana wa Haruni kuhani, amezigeuza hasira zangu zisiwe juu ya wana Wa Israeli, kwa kuwa alikuwa na wivu kati yao kwa wivu wangu mimi, hata nisiwaangamize wana wa Israeli katika wivu wangu.

12. Basi kwa hiyo, sema, Tazama, nampa yeye agano langu la amani;

Hes. 25