6. BWANA akatuma nyoka za moto kati ya watu, wakawauma, watu wengi wakafa.
7. Watu wakamwendea Musa, wakasema, Tumefanya dhambi kwa sababu tumemnung’unikia Mungu, na wewe; utuombee kwa BWANA, atuondolee nyoka hawa. Basi Musa akawaombea watu.
8. Bwana akamwambia Musa, Jifanyie nyoka ya shaba, ukaiweke juu ya mti, na itakuwa kila mtu aliyeumwa, aitazamapo ataishi.
9. Musa akafanya nyoka ya shaba, akaiweka juu ya mti, hata ikiwa nyoka amemwuma mtu, alipoitazama ile nyoka ya shaba, akaishi.
10. Kisha wana wa Israeli wakasafiri, wakapanga marago Obothi.
11. Wakasafiri kutoka Obothi, wakapanga Iye-abarimu, katika jangwa iliyoelekea Moabu, upande wa maawio ya jua.
12. Kutoka huko wakasafiri, wakapanga katika bonde la Zeredi.
13. Kutoka huko wakasafiri, wakapanga upande wa pili wa Arnoni, ulio jangwani, utokao katika mpaka wa Waamori; maana, Arnoni ndio mpaka wa Moabu, kati ya Moabu na Waamori.
14. Kwa hiyo imesemwa katika chuo cha Vita vya BWANA,Wahebu katika Sufa,Na bonde za Arnoni,
15. Na matelemko ya hizo bondeKwenye kutelemkia maskani ya Ari,Na kutegemea mpaka wa Moabu.
16. Kutoka huko wakasafiri kwenda Beeri; ni kisima ambacho BWANA alimwambia Musa, Uwakutanishe watu, nami nitawapa maji.
17. Ndipo Israeli wakaimba wimbo huu;Bubujika Ee kisima; kiimbieni;
18. Kisima walichokichimba wakuu,Ambacho wakuu wa watu wakakifukua,Kwa fimbo za enzi, kwa fimbo zao.Kutoka lile jangwa wakaenda Matana;
19. na kutoka Matana wakaenda Nahalieli; na kutoka Nahalieli wakaenda Bamothi;
20. na kutoka Bamothi wakaenda bondeni kwenye konde la Moabu, hata kilele cha Pisga, kielekeacho chini jangwani.
21. Kisha Israeli akatuma wajumbe kumwendea Sihoni mfalme wa Waamori, na kusema,
22. Nipe ruhusa nipite katika nchi yako; hatutageuka kando kwenda mashambani, wala kuingia katika mashamba ya mizabibu hatutakunywa maji ya visimani; tutakwenda kwa njia kuu ya mfalme, hata tutakapokuwa tumepita mpaka wako.
23. Lakini Sihoni hakukubali kumwacha Israeli kupita katika mpaka wake; bali Sihoni akawakutanisha watu wake wote, akatoka aende kupigana na Israeli jangwani, akafika mpaka Yahasa; akapigana na Israeli.
24. Israeli wakampiga kwa makali ya upanga, na kuimiliki nchi yake, tangu mto wa Arnoni hata mto wa Yaboki, mpaka nchi ya wana wa Amoni; kwa kuwa mpaka wa wana wa Amoni ulikuwa una nguvu.