Hes. 21:16-20 Swahili Union Version (SUV)

16. Kutoka huko wakasafiri kwenda Beeri; ni kisima ambacho BWANA alimwambia Musa, Uwakutanishe watu, nami nitawapa maji.

17. Ndipo Israeli wakaimba wimbo huu;Bubujika Ee kisima; kiimbieni;

18. Kisima walichokichimba wakuu,Ambacho wakuu wa watu wakakifukua,Kwa fimbo za enzi, kwa fimbo zao.Kutoka lile jangwa wakaenda Matana;

19. na kutoka Matana wakaenda Nahalieli; na kutoka Nahalieli wakaenda Bamothi;

20. na kutoka Bamothi wakaenda bondeni kwenye konde la Moabu, hata kilele cha Pisga, kielekeacho chini jangwani.

Hes. 21