Hes. 21:15-23 Swahili Union Version (SUV)

15. Na matelemko ya hizo bondeKwenye kutelemkia maskani ya Ari,Na kutegemea mpaka wa Moabu.

16. Kutoka huko wakasafiri kwenda Beeri; ni kisima ambacho BWANA alimwambia Musa, Uwakutanishe watu, nami nitawapa maji.

17. Ndipo Israeli wakaimba wimbo huu;Bubujika Ee kisima; kiimbieni;

18. Kisima walichokichimba wakuu,Ambacho wakuu wa watu wakakifukua,Kwa fimbo za enzi, kwa fimbo zao.Kutoka lile jangwa wakaenda Matana;

19. na kutoka Matana wakaenda Nahalieli; na kutoka Nahalieli wakaenda Bamothi;

20. na kutoka Bamothi wakaenda bondeni kwenye konde la Moabu, hata kilele cha Pisga, kielekeacho chini jangwani.

21. Kisha Israeli akatuma wajumbe kumwendea Sihoni mfalme wa Waamori, na kusema,

22. Nipe ruhusa nipite katika nchi yako; hatutageuka kando kwenda mashambani, wala kuingia katika mashamba ya mizabibu hatutakunywa maji ya visimani; tutakwenda kwa njia kuu ya mfalme, hata tutakapokuwa tumepita mpaka wako.

23. Lakini Sihoni hakukubali kumwacha Israeli kupita katika mpaka wake; bali Sihoni akawakutanisha watu wake wote, akatoka aende kupigana na Israeli jangwani, akafika mpaka Yahasa; akapigana na Israeli.

Hes. 21