4. Na jeshi lake, na wale waliohesabiwa kwao, walikuwa sabini na nne elfu na mia sita.
5. Na hao watakaopanga karibu naye ni kabila ya Isakari; na mkuu wa wana wa Isakari atakuwa Nethaneli mwana wa Suari;
6. na jeshi lake, na wale waliohesabiwa kwao, walikuwa hamsini na nne elfu na mia nne;
7. na kabila ya Zabuloni; na mkuu wa wana wa Zabuloni atakuwa Eliabu mwana wa Heloni;
8. na jeshi lake, na wale waliohesabiwa kwao, walikuwa hamsini na saba elfu na mia nne.