Hes. 15:31-39 Swahili Union Version (SUV)

31. Kwa sababu amelidharau neno la BWANA, na kuyavunja maagizo yake; mtu huyo atakatiliwa mbali, uovu wake utakuwa juu yake.

32. Kisha wakati huo wana wa Israeli walipokuwako jangwani, wakamwona mtu mmoja akikusanya kuni siku ya Sabato.

33. Hao waliomwona akikusanya kuni wakamleta kwa Musa na Haruni, na kwa mkutano wote.

34. Nao wakamweka kifungoni, maana, lilikuwa halijasemwa atakalotendwa.

35. BWANA akamwambia Musa, Mtu huyo lazima atauawa; mkutano wote watampiga kwa mawe huko nje ya marago.

36. Basi mkutano wote wakampeleka nje ya marago, nao wakampiga kwa mawe, akafa; kama BWANA alivyomwagiza Musa.

37. Kisha BWANA akasema na Musa, na kumwambia,

38. Nena na wana wa Israeli, na kuwaagiza ya kwamba wajifanyie vishada katika ncha za nguo zao, katika vizazi vyao, tena ya kwamba watie katika kila kishada cha kila ncha nyuzi za rangi ya samawi;

39. nacho kitakuwa kwenu ni kishada, ili mpate kukiangalia, na kuyakumbuka maagizo yote ya BWANA, na kuyafanya; tena kwamba msiende kutanga-tanga kuandama mioyo yenu wenyewe, na macho yenu wenyewe, ambayo mlikuwa mkiyaandama kwa uasherati hapo kwanza;

Hes. 15