Hes. 14:1-4 Swahili Union Version (SUV)

1. Mkutano wote wakapaza sauti zao wakalia; watu wakatoka machozi usiku ule.

2. Kisha wana wa Israeli wote wakamnung’unikia Musa na Haruni; mkutano wote wakawaambia, Ingekuwa heri kama tungalikufa katika nchi ya Misri, au, ingekuwa heri kama tungalikufa katika jangwa hili.

3. Mbona BWANA anatuleta mpaka nchi hii ili tuanguke kwa upanga? Wake zetu na watoto wetu watakuwa mateka; je! Si afadhali turudi Misri?

4. Wakaambiana, Na tumweke mtu mmoja awe akida, tukarudi Misri.

Hes. 14