Hes. 13:1-7 Swahili Union Version (SUV)

1. Kisha BWANA akanena na Musa, akamwambia,

2. Tuma watu, ili waende wakaipeleleze nchi ya Kanaani, niwapayo wana wa Israeli; katika kabila ya baba zao mtamtuma mtu mmoja, kila mtu na awe mkuu kati yao.

3. Basi Musa akawatuma kutoka nyika ya Parani kama alivyoagizwa na BWANA; wote walikuwa ni watu walio vichwa vya wana wa Israeli.

4. Na majina yao ni haya; katika kabila ya Reubeni, Shamua mwana Zakuri.

5. Katika kabila ya Simeoni, Shafati mwana wa Hori.

6. Katika kabila ya Yuda, Kalebu mwana wa Yefune.

7. Katika kabila ya Isakari, Igali mwana wa Yusufu.

Hes. 13