Hes. 1:3-11 Swahili Union Version (SUV)

3. tangu mwenye miaka ishirini umri wake, na zaidi, wote wawezao kutoka kwenenda vitani katika Israeli; wewe na Haruni mtawahesabu kwa kuandama majeshi yao.

4. Tena mtu mume mmoja wa kila kabila atakuwa pamoja nanyi; kila mmoja aliye kichwa cha nyumba ya baba zake.

5. Na majina ya hao waume watakaosimama pamoja nanyi ni haya; Wa Reubeni; Elisuri mwana wa Shedeuri.

6. Wa Simeoni; Shelumieli mwana wa Suri-shadai.

7. Wa Yuda; Nashoni mwana wa Aminadabu.

8. Wa Isakari; Nethaneli mwana wa Suari.

9. Wa Zabuloni; Eliabu mwana wa Heloni.

10. Katika wana wa Yusufu; wa Efraimu, Elishama mwana wa Amihudi; na wa Manase; Gamalieli mwana wa Pedasuri.

11. Wa Benyamini Abidani mwana wa Gideoni.

Hes. 1