Hab. 3:9-19 Swahili Union Version (SUV)

9. Uta wako ukafanywa wazi kabisa;Viapo walivyopewa kabila vilikuwa neno thabiti;Ukaipasua nchi kwa mito.

10. Milima ilikuona, ikaogopa;Gharika ya maji ikapita;Vilindi vikatoa sauti yake,Vikainua juu mikono yake.

11. Jua na mwezi vikasimama makaoni mwao;Mbele ya nuru ya mishale yako ilipotapakaa,Mbele ya mwangaza wa mkuki wako umeremetao.

12. Ulikwenda katikati ya nchi kwa ghadhabu;Ukawapura mataifa kwa hasira.

13. Ukatokea kwa ajili ya wokovu wa watu wako,Kwa ajili ya wokovu wa masihi wako;Ukakiponda kichwa cha nyumba ya waovu,Ukiuweka wazi msingi hata mwambani.

14. Ukakichoma kichwa cha mashujaa wake kwa fimbo zao wenyewe;Wakaja kama kisulisuli ili kunitawanya;Kama wakifurahi kuwameza maskini kwa siri.

15. Ukaikanyaga bahari kwa farasi zako,Chungu ya maji yenye nguvu.

16. Nikasikia, na tumbo langu likatetemeka,Midomo yangu ikatikisika kwa sauti ile;Ubovu ukaingia mifupani mwangu,Nikatetemeka katika mahali pangu;Ili nipate kuingoja ile siku ya dhiki,Kundi lao washambuliao wakweapo juu ya watu.

17. Maana mtini hautachanua maua,Wala mizabibuni hamtakuwa na matunda;Taabu ya mzeituni itakuwa bure,Na mashamba hayatatoa chakula;Zizini hamtakuwa na kundi,Wala vibandani hamtakuwa na kundi la ng’ombe;

18. Walakini nitamfurahia BWANANitamshangilia Mungu wa wokovu wangu.

19. YEHOVA, aliye BWANA, ni nguvu zangu,Yeye huifanya miguu yangu kuwa kama ya kulungu,Naye ataniendesha katika mahali pangu palipoinuka.

Hab. 3