8. Je! BWANA aliikasirikia mito?Je! Hasira yako ilikuwa juu ya mito,Au ghadhabu yako juu ya bahari,Hata ukapanda farasi zako,Katika magari yako ya wokovu?
9. Uta wako ukafanywa wazi kabisa;Viapo walivyopewa kabila vilikuwa neno thabiti;Ukaipasua nchi kwa mito.
10. Milima ilikuona, ikaogopa;Gharika ya maji ikapita;Vilindi vikatoa sauti yake,Vikainua juu mikono yake.
11. Jua na mwezi vikasimama makaoni mwao;Mbele ya nuru ya mishale yako ilipotapakaa,Mbele ya mwangaza wa mkuki wako umeremetao.
12. Ulikwenda katikati ya nchi kwa ghadhabu;Ukawapura mataifa kwa hasira.
13. Ukatokea kwa ajili ya wokovu wa watu wako,Kwa ajili ya wokovu wa masihi wako;Ukakiponda kichwa cha nyumba ya waovu,Ukiuweka wazi msingi hata mwambani.
14. Ukakichoma kichwa cha mashujaa wake kwa fimbo zao wenyewe;Wakaja kama kisulisuli ili kunitawanya;Kama wakifurahi kuwameza maskini kwa siri.
15. Ukaikanyaga bahari kwa farasi zako,Chungu ya maji yenye nguvu.
16. Nikasikia, na tumbo langu likatetemeka,Midomo yangu ikatikisika kwa sauti ile;Ubovu ukaingia mifupani mwangu,Nikatetemeka katika mahali pangu;Ili nipate kuingoja ile siku ya dhiki,Kundi lao washambuliao wakweapo juu ya watu.