Gal. 6:5-12 Swahili Union Version (SUV)

5. Maana kila mtu atalichukua furushi lake mwenyewe.

6. Mwanafunzi na amshirikishe mkufunzi wake katika mema yote.

7. Msidanganyike, Mungu hadhihakiwi; kwa kuwa cho chote apandacho mtu, ndicho atakachovuna.

8. Maana yeye apandaye kwa mwili wake, katika mwili wake atavuna uharibifu; bali yeye apandaye kwa Roho, katika Roho atavuna uzima wa milele.

9. Tena tusichoke katika kutenda mema; maana tutavuna kwa wakati wake, tusipozimia roho.

10. Kwa hiyo kadiri tupatavyo nafasi na tuwatendee watu wote mema; na hasa jamaa ya waaminio.

11. Tazameni ni kwa herufi gani kubwa nimewaandikia kwa mkono wangu mimi mwenyewe!

12. Wote watakao kuonekana ni wazuri kwa mambo ya mwili, ndio wanaowashurutisha kutahiriwa; makusudi wasiudhiwe kwa ajili ya msalaba wa Kristo, hilo tu.

Gal. 6