Gal. 5:5-11 Swahili Union Version (SUV)

5. Maana sisi kwa Roho tunalitazamia tumaini la haki kwa njia ya imani.

6. Maana katika Kristo Yesu kutahiriwa hakufai neno, wala kutokutahiriwa, bali imani itendayo kazi kwa upendo.

7. Mlikuwa mkipiga mbio vizuri; ni nani aliyewazuia msiitii kweli?

8. Kushawishi huku hakukutoka kwake yeye anayewaita ninyi.

9. Chachu kidogo huchachua donge zima.

10. Nina matumaini kwenu katika Bwana, ya kwamba hamtakuwa na nia ya namna nyingine. Lakini yeye anayewafadhaisha atachukua hukumu yake, awaye yote.

11. Nami, ndugu zangu ikiwa ninahubiri habari ya kutahiriwa, kwa nini ningali ninaudhiwa? Hapo kwazo la msalaba limebatilika!

Gal. 5