Gal. 5:2-5 Swahili Union Version (SUV)

2. Tazama, mimi Paulo nawaambia ninyi ya kwamba, mkitahiriwa, Kristo hatawafaidia neno.

3. Tena namshuhudia kila mtu atahiriwaye, kwamba ni wajibu wake kuitimiza torati yote.

4. Mmetengwa na Kristo, ninyi mtakao kuhesabiwa haki kwa sheria; mmeanguka na kutoka katika hali ya neema.

5. Maana sisi kwa Roho tunalitazamia tumaini la haki kwa njia ya imani.

Gal. 5