Gal. 4:26-29 Swahili Union Version (SUV)

26. Bali Yerusalemu wa juu ni mwungwana, naye ndiye mama yetu sisi.

27. Kwa maana imeandikwa,Furahi, wewe uliye tasa, usiyezaa;Paza sauti, ulie, wewe usiye na utungu;Maana watoto wake aliyeachwa pekee ni wengiKuliko wa huyo aliye na mume.

28. Basi, ndugu zangu, kama Isaka sisi tu watoto wa ahadi.

29. Lakini kama vile siku zile yule aliyezaliwa kwa mwili alivyomwudhi yule aliyezaliwa kwa Roho, ndivyo ilivyo na sasa.

Gal. 4