Gal. 3:4-9 Swahili Union Version (SUV)

4. Mmepatikana na mateso makubwa namna hii bure? Ikiwa ni bure kweli.

5. Basi, yeye awapaye Roho na kufanya miujiza kati yenu, je! Afanya hayo kwa matendo ya sheria, au kwa kusikia kunakotokana na imani?

6. Kama vile Ibrahimu alivyomwamini Mungu akahesabiwa haki.

7. Fahamuni basi, ya kuwa wale walio wa imani, hao ndio wana wa Ibrahimu.

8. Na andiko, kwa vile lilivyoona tangu zamani kwamba Mungu atawahesabia haki Mataifa kwa imani, lilimhubiri Ibrahimu habari njema zamani, kusema, Katika wewe Mataifa yote watabarikiwa.

9. Basi hao walio wa imani hubarikiwa pamoja na Ibrahimu aliyekuwa mwenye imani.

Gal. 3