22. Na pamoja na hayo uniwekee tayari mahali pa kukaa; maana nataraji ya kwamba kwa maombi yenu mtajaliwa kunipata.
23. Epafra, aliyefungwa pamoja nami katika Kristo Yesu, akusalimu;
24. na Marko, na Aristarko, na Dema, na Luka, watendao kazi pamoja nami.
25. Neema ya Bwana Yesu Kristo na iwe pamoja na roho zenu.