Flm. 1:22-25 Swahili Union Version (SUV)

22. Na pamoja na hayo uniwekee tayari mahali pa kukaa; maana nataraji ya kwamba kwa maombi yenu mtajaliwa kunipata.

23. Epafra, aliyefungwa pamoja nami katika Kristo Yesu, akusalimu;

24. na Marko, na Aristarko, na Dema, na Luka, watendao kazi pamoja nami.

25. Neema ya Bwana Yesu Kristo na iwe pamoja na roho zenu.

Flm. 1