1. Neno la BWANA likanijia, kusema,
2. Mwanadamu, toa unabii juu ya wachungaji wa Israeli, toa unabii, uwaambie, naam, hao wachungaji, Bwana MUNGU asema hivi; Ole wao wachungaji wa Israeli, wanaojilisha wenyewe; je! Haiwapasi wachungaji kuwalisha kondoo?
3. Mnawala walionona, mnajivika manyoya, mnawachinja walionona; lakini hamwalishi kondoo.