1. Neno la BWANA likanijia tena, kusema,
2. Na wewe, mwanadamu, mfanyie Tiro maombolezo;
3. umwambie Tiro, Ewe ukaaye penye maingilio ya bahari, uliye mchuuzi wa watu wa kabila nyingi, mpaka visiwa vingi, Bwana MUNGU asema hivi; Wewe, Tiro, umesema, Mimi ni ukamilifu wa uzuri.
4. Mipaka yako i kati ya moyo wa bahari; wajenzi wako wameukamilisha uzuri wako.
5. Mbao zako zote wamezifanya kwa misunobari itokayo Seniri; wametwaa mierezi ya Lebanoni ili kukufanyia mlingoti;