Eze. 26:1-3 Swahili Union Version (SUV)

1. Ikawa katika mwaka wa kumi na mmoja, siku ya kwanza ya mwezi, neno la BWANA likanijia, kusema,

2. Mwanadamu, Kwa sababu Tiro amesema juu ya Yerusalemu, Aha! Yeye amevunjika aliyekuwa lango la kabila za watu; amenigeukia; nitajazwa kwa kuwa sasa ameharibika;

3. basi Bwana MUNGU asema hivi; Tazama, mimi ni juu yako, Ee Tiro, nami nitaleta mataifa mengi kupigana nawe, kama bahari iinuavyo mawimbi yake.

Eze. 26