Eze. 23:12-14 Swahili Union Version (SUV)

12. Aliwapendelea Waashuri, maliwali na mawaziri, jirani zake, waliovikwa nguo za shani, wapanda farasi wakipanda farasi zao, wote pia vijana wa kutamanika.

13. Nikaona ya kuwa ametiwa unajisi; wote wawili walifuata njia moja.

14. Naye akaongeza uzinzi wake; kwa maana aliona watu waume, ambao sura zao zimeandikwa ukutani, sura za Wakaldayo zilizoandikwa kwa rangi nyekundu;

Eze. 23