1. Neno la BWANA likanijia, kusema,
2. Mwanadamu, tega kitendawili, ukawaambie nyumba ya Israeli mithali;
3. useme, Bwana MUNGU asema hivi; Tai mkubwa, mwenye mabawa makubwa na manyoya marefu katika mabawa, mwenye kujaa manyoya, yaliyo ya rangi mbalimbali, alifika Lebanoni, akakitwaa kilele cha mwerezi;