Eze. 16:61-63 Swahili Union Version (SUV)

61. Hapo ndipo utakapozikumbuka njia zako, na kutahayarika, hapo utakapowakaribisha maumbu yako, walio wakubwa wako na wadogo wako; nami nitakupa hao wawe binti zako, lakini si kwa agano lako.

62. Nami nitaweka imara agano langu nawe; nawe utajua ya kuwa mimi ndimi BWANA;

63. upate kukumbuka, na kufadhaika, usifumbue kinywa chako tena, kwa sababu ya aibu yako; hapo nitakapokusamehe yote uliyoyatenda, asema Bwana MUNGU.

Eze. 16