21. hata ukawaua watoto wangu, na kuwatoa kwa kuwapitisha motoni kwa hao?
22. Na katika machukizo yako yote, na mambo yako ya kikahaba, hukuzikumbuka siku za ujana wako, ulipokuwa uchi, huna nguo, ukawa ukigaagaa katika damu yako.
23. Tena, imekuwa baada ya uovu wako wote, (ole wako! ole wako! Asema Bwana MUNGU,)
24. ulijijengea mahali palipoinuka, ukajifanyia mahali palipoinuka katika kila njia kuu.