Eze. 16:1-4 Swahili Union Version (SUV)

1. Neno la BWANA likanijia tena, kusema,

2. Mwanadamu, uujulishe Yerusalemu machukizo yake,

3. useme, Bwana MUNGU auambia Yerusalemu hivi; Asili yako na kuzaliwa kwako kwatoka katika nchi ya Mkanaani; Mwamori alikuwa baba yako, na mama yako alikuwa Mhiti.

4. Na katika habari za kuzaliwa kwako, siku ile uliyozaliwa, kitovu chako hakikukatwa, wala hukuoshwa kwa maji usafishwe; hukutiwa chumvi hata kidogo, wala hukutiwa katika nguo kabisa.

Eze. 16