1. Neno la BWANA likanijia tena, kusema,
2. Mwanadamu, uujulishe Yerusalemu machukizo yake,
3. useme, Bwana MUNGU auambia Yerusalemu hivi; Asili yako na kuzaliwa kwako kwatoka katika nchi ya Mkanaani; Mwamori alikuwa baba yako, na mama yako alikuwa Mhiti.