1. Kisha neno la BWANA likanijia, kusema,
2. Mwanadamu, tabiri juu ya manabii wa Israeli wanaotabiri, uwaambie wanaotabiri kwa mioyo yao wenyewe, Lisikieni neno la BWANA;
3. Bwana MUNGU asema hivi; Ole wao manabii wajinga, wanaoifuata roho yao wenyewe, wala hawakuona neno lo lote!
4. Ee Israeli, manabii wako wamekuwa kama mbweha, mahali palipo ukiwa.