Eze. 11:3-9 Swahili Union Version (SUV)

3. wasemao, Wakati wa kujenga nyumba si karibu; mji huu ni sufuria na sisi ni nyama.

4. Basi toa unabii juu yao, Ee mwanadamu, toa unabii.

5. Roho ya BWANA ikaniangukia, naye akaniambia, Nena, BWANA asema hivi; Mmesema maneno hayo, Enyi nyumba ya Israeli; maana mimi nayajua yaingiayo katika mioyo yenu.

6. Mmewaongeza watu wenu waliouawa ndani ya mji wenu, nanyi mmezijaza njia kuu zake waliouawa.

7. Basi Bwana MUNGU asema hivi; Watu wenu waliouawa, ambao mmewalaza katikati yake, hao ndio nyama hiyo, na mji huu ndio sufuria; lakini ninyi mtatolewa nje kutoka katikati yake.

8. Ninyi mmeuogopa upanga; nami nitauleta upanga juu yenu, asema Bwana MUNGU.

9. Nami nitawatoa ninyi nje kutoka katikati yake, na kuwatia katika mikono ya wageni, nami nitafanya hukumu kati yenu.

Eze. 11