5. Basi Wayahudi wakawapiga adui zao wote mapigo ya upanga, na machinjo, na maangamizo, wakawatenda kama wapendavyo wale waliowachukia.
6. Hata huko Shushani ngomeni Wayahudi wakawaua watu mia tano, na kuwaangamiza.
7. Wakawaua na Parshandatha, na Dalfoni, na Aspatha,
8. na Poratha, na Adalia, na Aridatha,
9. na Parmashta, na Arisai, na Aridai, na Waizatha,
10. wana kumi wa Hamani bin Hamedatha, adui ya Wayahudi; walakini juu ya nyara hawakuweka mikono.
11. Siku ile mfalme akaletewa hesabu ya hao waliouawa huko Shushani ngomeni.