1. Enyi watoto, watiini wazazi wenu katika Bwana, maana hii ndiyo haki.
2. Waheshimu baba yako na mama yako; amri hii ndiyo amri ya kwanza yenye ahadi,
3. Upate heri, ukae siku nyingi katika dunia.
4. Nanyi, akina baba, msiwachokoze watoto wenu; bali waleeni katika adabu na maonyo ya Bwana.