Efe. 5:8-13 Swahili Union Version (SUV)

8. Kwa maana zamani ninyi mlikuwa giza, bali sasa mmekuwa nuru katika Bwana; enendeni kama watoto wa nuru,

9. kwa kuwa tunda la nuru ni katika wema wote na haki na kweli;

10. mkihakiki ni nini impendezayo Bwana.

11. Wala msishirikiane na matendo yasiyozaa ya giza, bali myakemee;

12. kwa kuwa yanayotendeka kwao kwa siri, ni aibu hata kuyanena.

13. Lakini yote yaliyokemewa hudhihirishwa na nuru maana kila kilichodhihirika ni nuru.

Efe. 5