Efe. 4:17-24 Swahili Union Version (SUV)

17. Basi nasema neno hili, tena nashuhudia katika Bwana, tangu sasa msienende kama Mataifa waenendavyo, katika ubatili wa nia zao;

18. ambao; akili zao zimetiwa giza, nao wamefarikishwa na uzima wa Mungu, kwa sababu ya ujinga uliomo ndani yao, kwa sababu ya ugumu wa mioyo yao;

19. ambao wakiisha kufa ganzi wanajitia katika mambo ya ufisadi wapate kufanyiza kila namna ya uchafu kwa kutamani.

20. Bali ninyi, sivyo mlivyojifunza Kristo;

21. ikiwa mlimsikia mkafundishwa katika yeye, kama kweli ilivyo katika Yesu,

22. mvue kwa habari ya mwenendo wa kwanza utu wa zamani, unaoharibika kwa kuzifuata tamaa zenye kudanganya;

23. na mfanywe wapya katika roho ya nia zenu;

24. mkavae utu mpya, ulioumbwa kwa namna ya Mungu katika haki na utakatifu wa kweli.

Efe. 4