17. Basi nasema neno hili, tena nashuhudia katika Bwana, tangu sasa msienende kama Mataifa waenendavyo, katika ubatili wa nia zao;
18. ambao; akili zao zimetiwa giza, nao wamefarikishwa na uzima wa Mungu, kwa sababu ya ujinga uliomo ndani yao, kwa sababu ya ugumu wa mioyo yao;
19. ambao wakiisha kufa ganzi wanajitia katika mambo ya ufisadi wapate kufanyiza kila namna ya uchafu kwa kutamani.
20. Bali ninyi, sivyo mlivyojifunza Kristo;
21. ikiwa mlimsikia mkafundishwa katika yeye, kama kweli ilivyo katika Yesu,
22. mvue kwa habari ya mwenendo wa kwanza utu wa zamani, unaoharibika kwa kuzifuata tamaa zenye kudanganya;
23. na mfanywe wapya katika roho ya nia zenu;
24. mkavae utu mpya, ulioumbwa kwa namna ya Mungu katika haki na utakatifu wa kweli.