5. Kwa hiyo ajapo ulimwenguni, asema,Dhabihu na toleo hukutaka,Lakini mwili uliniwekea tayari;
6. Sadaka za kuteketezwa na sadaka za dhambi hukupendezwa nazo;
7. Ndipo niliposema, Tazama, nimekuja (katika gombo la chuo nimeandikiwa)Niyafanye mapenzi yako, Mungu.
8. Hapo juu asemapo, Dhabihu na matoleo na sadaka za kuteketezwa na hizo za dhambi hukuzitaka, wala hukupendezwa nazo (zitolewazo kama ilivyoamuru torati),
9. ndipo aliposema, Tazama, nimekuja niyafanye mapenzi yako. Aondoa la kwanza, ili kusudi alisimamishe la pili.
10. Katika mapenzi hayo mmepata utakaso, kwa kutolewa mwili wa Yesu Kristo mara moja tu.
11. Na kila kuhani husimama kila siku akifanya ibada, na kutoa dhabihu zile zile mara nyingi; ambazo haziwezi kabisa kuondoa dhambi.
12. Lakini huyu, alipokwisha kutoa kwa ajili ya dhambi dhabihu moja idumuyo hata milele, aliketi mkono wa kuume wa Mungu;
13. tangu hapo akingojea hata adui zake wawekwe kuwa chini ya miguu yake.
14. Maana kwa toleo moja amewakamilisha hata milele hao wanaotakaswa.
15. Na Roho Mtakatifu naye amshuhudia; kwa maana, baada ya kusema,
16. Hili ni agano nitakaloagana nao baada ya siku zile, anena Bwana,Nitatia sheria zangu mioyoni mwao,Na katika nia zao nitaziandika;ndipo anenapo,
17. Dhambi zao na uasi wao sitaukumbuka tena kabisa.
18. Basi, ondoleo la hayo likiwapo, hapana toleo tena kwa ajili ya dhambi.
19. Basi, ndugu, kwa kuwa tuna ujasiri wa kupaingia patakatifu kwa damu ya Yesu,
20. njia ile aliyotuanzia iliyo mpya, iliyo hai, ipitayo katika pazia, yaani, mwili wake;
21. na kuwa na kuhani mkuu juu ya nyumba ya Mungu;
22. na tukaribie wenye moyo wa kweli, kwa utimilifu wa imani, hali tumenyunyiziwa mioyo tuache dhamiri mbaya, tumeoshwa miili kwa maji safi.
23. Na mlishike sana ungamo la tumaini letu, lisigeuke; maana yeye aliyeahidi ni mwaminifu;