Ebr. 10:14-19 Swahili Union Version (SUV)

14. Maana kwa toleo moja amewakamilisha hata milele hao wanaotakaswa.

15. Na Roho Mtakatifu naye amshuhudia; kwa maana, baada ya kusema,

16. Hili ni agano nitakaloagana nao baada ya siku zile, anena Bwana,Nitatia sheria zangu mioyoni mwao,Na katika nia zao nitaziandika;ndipo anenapo,

17. Dhambi zao na uasi wao sitaukumbuka tena kabisa.

18. Basi, ondoleo la hayo likiwapo, hapana toleo tena kwa ajili ya dhambi.

19. Basi, ndugu, kwa kuwa tuna ujasiri wa kupaingia patakatifu kwa damu ya Yesu,

Ebr. 10