Ayu. 9:29-35 Swahili Union Version (SUV)

29. Nitahukumiwa kuwa ni mkosa;Ya nini basi nitaabike bure?

30. Ingawaje najiosha kwa maji ya theluji,Na kuitakasa mikono yangu kwa sabuni;

31. Lakini utanitupa shimoni,Nami hata nguo zangu zitanichukia.

32. Kwani yeye si mtu, kama mimi, hata nimjibu,Hata tukaribiane katika hukumu.

33. Hapana mwenye kuamua katikati yetu,Awezaye kutuwekea mkono sote wawili.

34. Na aniondolee fimbo yake,Na utisho wake usinitie hofu;

35. Ndipo hapo ningesema, nisimwogope;Kwani sivyo nilivyo nafsini mwangu.

Ayu. 9