25. Basi siku zangu zina mbio kuliko tarishi;Zakimbia, wala hazioni mema.
26. Zimepita kama merikebu ziendazo mbio;Mfano wa tai ayashukiaye mawindo.
27. Nikisema, Mimi nitasahau kuugua kwangu,Nitaacha kununa uso nikachangamke moyo;
28. Mimi huziogopa huzuni zangu zote,Najua kuwa hutanihesabu kuwa sina hatia.