Ayu. 9:24-33 Swahili Union Version (SUV)

24. Dunia imetiwa mkononi mwa waovu;Yeye hufunika nyuso za waamuzi wake;Kama si yeye, ni nani basi?

25. Basi siku zangu zina mbio kuliko tarishi;Zakimbia, wala hazioni mema.

26. Zimepita kama merikebu ziendazo mbio;Mfano wa tai ayashukiaye mawindo.

27. Nikisema, Mimi nitasahau kuugua kwangu,Nitaacha kununa uso nikachangamke moyo;

28. Mimi huziogopa huzuni zangu zote,Najua kuwa hutanihesabu kuwa sina hatia.

29. Nitahukumiwa kuwa ni mkosa;Ya nini basi nitaabike bure?

30. Ingawaje najiosha kwa maji ya theluji,Na kuitakasa mikono yangu kwa sabuni;

31. Lakini utanitupa shimoni,Nami hata nguo zangu zitanichukia.

32. Kwani yeye si mtu, kama mimi, hata nimjibu,Hata tukaribiane katika hukumu.

33. Hapana mwenye kuamua katikati yetu,Awezaye kutuwekea mkono sote wawili.

Ayu. 9