24. Dunia imetiwa mkononi mwa waovu;Yeye hufunika nyuso za waamuzi wake;Kama si yeye, ni nani basi?
25. Basi siku zangu zina mbio kuliko tarishi;Zakimbia, wala hazioni mema.
26. Zimepita kama merikebu ziendazo mbio;Mfano wa tai ayashukiaye mawindo.
27. Nikisema, Mimi nitasahau kuugua kwangu,Nitaacha kununa uso nikachangamke moyo;
28. Mimi huziogopa huzuni zangu zote,Najua kuwa hutanihesabu kuwa sina hatia.
29. Nitahukumiwa kuwa ni mkosa;Ya nini basi nitaabike bure?
30. Ingawaje najiosha kwa maji ya theluji,Na kuitakasa mikono yangu kwa sabuni;
31. Lakini utanitupa shimoni,Nami hata nguo zangu zitanichukia.
32. Kwani yeye si mtu, kama mimi, hata nimjibu,Hata tukaribiane katika hukumu.
33. Hapana mwenye kuamua katikati yetu,Awezaye kutuwekea mkono sote wawili.