22. Hayo yote ni mamoja; kwa hiyo nasema,Yeye huangamiza wakamilifu na waovu pia.
23. Kama hilo pigo likiua ghafula,Atayadhihaki majaribu yake asiye na kosa.
24. Dunia imetiwa mkononi mwa waovu;Yeye hufunika nyuso za waamuzi wake;Kama si yeye, ni nani basi?
25. Basi siku zangu zina mbio kuliko tarishi;Zakimbia, wala hazioni mema.
26. Zimepita kama merikebu ziendazo mbio;Mfano wa tai ayashukiaye mawindo.
27. Nikisema, Mimi nitasahau kuugua kwangu,Nitaacha kununa uso nikachangamke moyo;