Ayu. 9:19-23 Swahili Union Version (SUV)

19. Kama tukitaja nguvu za mashujaa, tazama yupo hapo!Kama tukitaja hukumu, ni nani atakayeniwekea muhula?

20. Ingawa ni mwenye haki, kinywa changu mwenyewe kitanihukumu;Ingawa ni mkamilifu, kitanishuhudia kuwa ni mpotovu.

21. Mimi ni mkamilifu; siangalii nafsi yangu;Naudharau uhai wangu.

22. Hayo yote ni mamoja; kwa hiyo nasema,Yeye huangamiza wakamilifu na waovu pia.

23. Kama hilo pigo likiua ghafula,Atayadhihaki majaribu yake asiye na kosa.

Ayu. 9