12. Tazama, yuakamata, ni nani awezaye kumzuia?Ni nani awezaye kumwuliza, Wafanya nini?
13. Mungu haondoi hasira zake;Hao wamsaidiao Rahabu huinama chini yake.
14. Je! Mimi nitamjibuje,Na kuyachagua maneno yangu kuhojiana naye?
15. Ambaye, nijapokuwa mimi ni mwenye haki, nisingemjibu;Ningemsihi-sihi mtesi wangu.
16. Kama ningemwita, naye akaniitikia;Hata hivyo singeamini kuwa amesikiza sauti yangu.
17. Yeye anipondaye kwa dhoruba,Na kuziongeza jeraha zangu pasipokuwa na sababu.
18. Haniachi nipate kuvuta pumzi,Lakini hunijaza uchungu.
19. Kama tukitaja nguvu za mashujaa, tazama yupo hapo!Kama tukitaja hukumu, ni nani atakayeniwekea muhula?
20. Ingawa ni mwenye haki, kinywa changu mwenyewe kitanihukumu;Ingawa ni mkamilifu, kitanishuhudia kuwa ni mpotovu.
21. Mimi ni mkamilifu; siangalii nafsi yangu;Naudharau uhai wangu.
22. Hayo yote ni mamoja; kwa hiyo nasema,Yeye huangamiza wakamilifu na waovu pia.
23. Kama hilo pigo likiua ghafula,Atayadhihaki majaribu yake asiye na kosa.
24. Dunia imetiwa mkononi mwa waovu;Yeye hufunika nyuso za waamuzi wake;Kama si yeye, ni nani basi?