10. Atendaye mambo makuu yasiyotafutikana;Naam, mambo ya ajabu yasiyohesabika.
11. Tazama, yuaenenda karibu nami, nisimwone;Tena yuapita kwenda mbele, nisimtambue.
12. Tazama, yuakamata, ni nani awezaye kumzuia?Ni nani awezaye kumwuliza, Wafanya nini?
13. Mungu haondoi hasira zake;Hao wamsaidiao Rahabu huinama chini yake.
14. Je! Mimi nitamjibuje,Na kuyachagua maneno yangu kuhojiana naye?
15. Ambaye, nijapokuwa mimi ni mwenye haki, nisingemjibu;Ningemsihi-sihi mtesi wangu.
16. Kama ningemwita, naye akaniitikia;Hata hivyo singeamini kuwa amesikiza sauti yangu.
17. Yeye anipondaye kwa dhoruba,Na kuziongeza jeraha zangu pasipokuwa na sababu.