Ayu. 9:10-17 Swahili Union Version (SUV)

10. Atendaye mambo makuu yasiyotafutikana;Naam, mambo ya ajabu yasiyohesabika.

11. Tazama, yuaenenda karibu nami, nisimwone;Tena yuapita kwenda mbele, nisimtambue.

12. Tazama, yuakamata, ni nani awezaye kumzuia?Ni nani awezaye kumwuliza, Wafanya nini?

13. Mungu haondoi hasira zake;Hao wamsaidiao Rahabu huinama chini yake.

14. Je! Mimi nitamjibuje,Na kuyachagua maneno yangu kuhojiana naye?

15. Ambaye, nijapokuwa mimi ni mwenye haki, nisingemjibu;Ningemsihi-sihi mtesi wangu.

16. Kama ningemwita, naye akaniitikia;Hata hivyo singeamini kuwa amesikiza sauti yangu.

17. Yeye anipondaye kwa dhoruba,Na kuziongeza jeraha zangu pasipokuwa na sababu.

Ayu. 9