Ayu. 9:1-4 Swahili Union Version (SUV)

1. Ndipo Ayubu akajibu, na kusema,

2. Kweli najua kuwa ndivyo hivyo;Lakini mtu huwaje mwenye haki mbele za Mungu?

3. Kama akipenda kushindana naye,Hawezi kumjibu neno moja katika elfu.

4. Yeye ni mwenye hekima moyoni, na mwenye uwezo katika nguvu;Ni nani aliyejifanya kuwa mgumu juu yake, naye akafanikiwa?

Ayu. 9