1. Ndipo Ayubu akajibu, na kusema,
2. Kweli najua kuwa ndivyo hivyo;Lakini mtu huwaje mwenye haki mbele za Mungu?
3. Kama akipenda kushindana naye,Hawezi kumjibu neno moja katika elfu.
4. Yeye ni mwenye hekima moyoni, na mwenye uwezo katika nguvu;Ni nani aliyejifanya kuwa mgumu juu yake, naye akafanikiwa?