Ayu. 7:9-14 Swahili Union Version (SUV)

9. Kama vile wingu likomavyo na kutoweka,Ni vivyo huyo ashukaye kuzimuni hatazuka tena kabisa.

10. Hatarudi tena nyumbani kwake,Wala mahali pake hapatamjua tena.

11. Kwa hiyo sitakizuia kinywa changu;Nitanena kwa mateso ya roho yangu;Nitalia kwa uchungu wa nafsi yangu.

12. Je! Mimi ni bahari, au je! Ni nyangumi?Hata ukawaweka walinzi juu yangu?

13. Hapo nisemapo, kitanda changu kitanituza moyo,Malazi yangu yatanipunguzia kuugua kwangu;

14. Ndipo unitishapo kwa ndoto,Na kunitia hofu kwa maono;

Ayu. 7