Ayu. 7:2-7 Swahili Union Version (SUV)

2. Kama mtumishi atamaniye sana kile kivuli,Kama mwajiriwa anayetazamia mshahara wake;

3. Ni vivyo nami nimepewa miezi ya ubatili iwe fungu langu,Nami nimeandikiwa masiku yenye kuchokesha.

4. Hapo nilalapo chini, nasema,Nitaondoka lini? Lakini usiku huwa mrefu;Nami nimejawa na kujitupa huku na huku hata kupambazuke.

5. Mwili wangu unavikwa mabuu na madongoa ya udongo;Ngozi yangu hufumba, kisha ikatumbuka tena.

6. Siku zangu hupita upesi kuliko chombo cha kufumia,Nazo zapita pasipokuwa na matumaini.

7. Kumbuka ya kwamba maisha yangu ni upepo;Jicho langu halitaona mema tena.

Ayu. 7