17. Je! Mtu ni kitu gani, hata ukamtukuza,Na kumtia moyoni mwako,
18. Na kumwangalia kila asubuhi,Na kumjaribu kila dakika?
19. Je! Hata lini hukomi kuniangalia;Wala kunisumbua hata nimeze mate?
20. Kwamba nimefanya dhambi, nikufanyieje Ee mlinda wanadamu?Mbona umeniweka niwe shabaha yako,Hata nimekuwa mzigo kwa nafsi yangu?