Ayu. 7:17-20 Swahili Union Version (SUV)

17. Je! Mtu ni kitu gani, hata ukamtukuza,Na kumtia moyoni mwako,

18. Na kumwangalia kila asubuhi,Na kumjaribu kila dakika?

19. Je! Hata lini hukomi kuniangalia;Wala kunisumbua hata nimeze mate?

20. Kwamba nimefanya dhambi, nikufanyieje Ee mlinda wanadamu?Mbona umeniweka niwe shabaha yako,Hata nimekuwa mzigo kwa nafsi yangu?

Ayu. 7