11. Kwa hiyo sitakizuia kinywa changu;Nitanena kwa mateso ya roho yangu;Nitalia kwa uchungu wa nafsi yangu.
12. Je! Mimi ni bahari, au je! Ni nyangumi?Hata ukawaweka walinzi juu yangu?
13. Hapo nisemapo, kitanda changu kitanituza moyo,Malazi yangu yatanipunguzia kuugua kwangu;
14. Ndipo unitishapo kwa ndoto,Na kunitia hofu kwa maono;
15. Hata nafsi yangu huchagua kunyongwa,Na kuchagua kifo kuliko maumivu yangu haya.
16. Ninadhoofika; sitaishi sikuzote;Usinisumbue, kwani siku zangu ni uvuvio.
17. Je! Mtu ni kitu gani, hata ukamtukuza,Na kumtia moyoni mwako,
18. Na kumwangalia kila asubuhi,Na kumjaribu kila dakika?