Ayu. 7:11-18 Swahili Union Version (SUV)

11. Kwa hiyo sitakizuia kinywa changu;Nitanena kwa mateso ya roho yangu;Nitalia kwa uchungu wa nafsi yangu.

12. Je! Mimi ni bahari, au je! Ni nyangumi?Hata ukawaweka walinzi juu yangu?

13. Hapo nisemapo, kitanda changu kitanituza moyo,Malazi yangu yatanipunguzia kuugua kwangu;

14. Ndipo unitishapo kwa ndoto,Na kunitia hofu kwa maono;

15. Hata nafsi yangu huchagua kunyongwa,Na kuchagua kifo kuliko maumivu yangu haya.

16. Ninadhoofika; sitaishi sikuzote;Usinisumbue, kwani siku zangu ni uvuvio.

17. Je! Mtu ni kitu gani, hata ukamtukuza,Na kumtia moyoni mwako,

18. Na kumwangalia kila asubuhi,Na kumjaribu kila dakika?

Ayu. 7